Na Humphrey Shao,Michuzi
MWENYEKITI wa Umoja wa wanawake Tanzania UWT, Mary Chatanda, leo Desemba 16, 2023 amezindua Kamati ya Mapambano dhidi ya ukatili wa Wanawake na Watoto.

Akizindua kamati hiyo katika Viwanja vya Mnazi Mmmoja Jijini Dar es Salaam leo, Bi Chatanda amesema uundwaji wa kamati hii ni kutokana na Maelekezo ya Mh. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika hotuba yake kwenye mkutano wa UWT Dodoma.

"Majukumu ya kamati hii ni kuweka Mikakati ya kushughulikia na kutokomeza vitendo vya ukakatili uzalilishaji kwa wanawake na watoto kama vile ubakaji na ulawiti." Amesema Chatanda

Pia ametoa maelekezo kwa kuhakikisha mikoa inaunda kamati ya Mapambano dhidi ya ukatili kwenye ngazi zote za Uongozi na kupanga Ratiba ya Viongozi wa UWT kutembelea madawati ya jinsia na kuhakikisha taarifa ya kesi za ukatili na hatua zilizofikia zinawasilishwa makao makuu.

Amesema pia kamati hiyo itaweza kuishauri kamati ya msaada wa kisheria kesi ambazo zinahitaji msaada wa kisheria kutoka UWT.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...