Na, Brow Jonas - WUSM

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro amesema Serikali itazindua Tuzo ya Kimataifa ya Kiswahili kwa Hayati Mwl. Julius Kambarage Nyerere ili kuenzi mchango wake katika kukuza Kiswahili duniani

Mhe. Ndumbaro amesema hayo leo Desemba 15, 2023 wakati wa  kongamano la 8 la Kiswahili lililoandaliwa na Chama Cha Ukuzaji Kiswahili Duniani (CHAUKIDU) Jijini Arusha.

Mhe. Ndumbaro amesema tuzo hizo zitatolewa katika makao makuu ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini Ufaransa ikiwa ni heshima ya Shirika hilo kuitambua lugha ya Kiswahili duniani na kutenga  Julai 7 kila mwaka kuwa siku ya Kiswahili duniani.

Ameongeza kuwa katika tuzo pia watu wengine waliojitoa kukuza Kiswahili watatambuliwa na kupewa tuzo kwa heshima ya Baba wa Taifa

Kongamano hilo limehudhuriwa na washiriki kutoka mataifa mbalimbali duniani ikiwemo Ufaransa, Marekani, Malawi, Kenya na Uganda ambapo mijadala mbalimbali ya kubidhaisha Kiswahili imejadiliwa.



 





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...