NA
K-VIS BLOG/KHALFAN SAID, MOSHI
KAIMU
Katibu Tawala Mkoa wa Kilimanjaro, ambaye pia ni Mganga Mkuu wa Mkoa huo, Dkt.
Jairy Khanga, amesema madaktari wanaofanya Tathmini za Ulemavu na Magonjwa
yatokanayo na Kazi, wanapaswa kufanya kazi hiyo kwa uadilifu ili wanaostahili
waweze kupata fidia stahiki na kwa wakati.
Dkt.
Khanga, ameyasema hayo Desemba 8, 2023, wakati akifunga mafunzo ya siku tano ya
Tathmini za Ulemavu na Magonjwa yatokanayo na Kazi kwa madaktari wa mikoa ya Kanda ya Kaskazini inayojumuisha Tanga, Kilimanjaro, Arusha na Manyara na
kufanyika kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, mjini Moshi.
“Sisi
tukiwa watarajiwa wa fidia, lazima tuhakikishe haki inayotakiwa kutolewa kwa
mwenzetu ambaye amepata ajali kwa bahati mbaya au ameugua kutokana na mazingira ya kazi yake, basi twende tukaifanye kazi hiyo kwa weledi
mkubwa.” Amefafanua Dkt. Khanga.
Amesema
matarajio ya WCF lakini pia Serikali, ni kuona mafunzo waliyopata washiriki yanawasaidia kufanya tathmini
uhakika ambayo haina mgongano wa maslahi kwa mtu mmoja mmoja au kikundi
cha watu.
Vilevile ni matarajio ya mfanyakazi aliyeumia au kuugua kutokana na kazi, kuwa atapata fidia anayostahili bila manung’uniko, amesema.
Kwa
upande wake, Mkurugenzi wa Huduma za Tathmini, WCF, Dkt. Abdulsalaam Omar,
amesema, Mfuko umepanua wigo wa kutoa mafunzo ya Tathmini za Ulemavu na
Magonjwa yatokanayo na Kazi kwa Madaktari kuanzia
ngazi ya Vituo vya Afya hadi Hospitali za Rufaa za Kanda.
“Kama alivyosema
Mkurugenzi Mkuu wakati wa ufunguzi wa mafunzo haya, lengo letu ni
kwamba, kila mfanyakazi, mahali popote alipo, endapo ataumia au kuugua kutokana
na kazi, apate fidia stahiki na kwa wakati kwa mujibu wa sheria ya fidia kwa wafanyakazi.”
Amesisitiza Dkt. Omar.
Amesema, Mafunzo hayo yanawawezesha madaktari kupata uelewa wa Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi, ikiwa ni pamoja na kufanya tathmini sahihi ili hatimaye mlengwa apate anachostahili, bila kumzidishia au kumpunguzia.
Akizungumza
kwa niaba ya washiriki wengine, Dkt. Kisse Kamwela, amemshukuru Rais wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuendelea kuwekeza
kwenye Mfuko na hivyo kuweza kutekeleza majukumu yake ikiwemo kutoa elimu ya
fidia kwa makundi mbalimbali, madaktari wakiwemo.
“Mimi
kama Mfanyakazi, ninanufaika na Mfuko huu, mafunzo haya yameniwezesha kujua
haki zangu kama mfanyakazi, lakini kama daktari nimejifunza namna ya kumuhudumia
mgonjwa aliyepata changamoto kutokana na kazi” amesema.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...