Na Yeremias Ngerangera...Namtumbo

Baraza la madiwani la Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo limepokea Mapendekezo ya kuanzisha vyanzo vipya vya mapato kwa lengo la kuongeza mapato ya ndani.

Diwani wa kata ya Mkongo Daniel Nyambo alisema Mapendekezo hayo ya kuanzisha vyanzo vipya vya mapato ni mazuri lakini akaomba madiwani wapate muda wa kupitia vyanzo hivyo na baraza lijalo waweze Kutoa maamuzi.

Lukas Njogopa Diwani wa kata ya Rwinga naye Kwa upande wake alisema kuwa ni vyema waheshimiwa madiwani wakapitie vyanzo hivyo vya mapato Ili baraza lijalo waje na maamuzi mazuri

Katibu kamati ya mapato na afisa mipango na uratibu wa Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo Musa Mumina katika taarifa yake kwenye baraza Hilo alifafanua vyanzo vipya vya mapato vinavyopendekezwa ni pamoja na ujenzi wa vibanda vya biashara,ujenzi wa karakana ya magari na mitambo,mashine ya kufuatilia tofali za saruji.,kiwanda Cha maji ya chupa na ujenzi wa shule ya Sekondari.

Hata hivyo aliongeza kuvitaja vyanzo vingine kuwa ni ununuzi wa mashine ya kuchakata kokoto,ujenzi wa ghala la kuhifadhia mazao,ujenzi wa stendi ndogondogo kwenye ngazi ya kata na vijiji pamoja na kituo Cha kuuza mafuta(Petrol station)

Amandus Chilumba afisa Serikali za mitaa kutoka ofisi ya mkuu wa Mkoa wa Ruvuma aliwataka waheshimiwa madiwani Kushirikiana na wataalamu katika zoezi la ukusanyaji wa mapato.,mapato ndio uhai wa Halmashauri alisema Chilumba.

Chilumba pia alisisitiza kudumisha mahusiano ili kushughulikia mambo Kwa hekima, busara na akili katika kutatua changamoto zinazohitajika kutatuliwa .

Mapendekezo ya vyanzo vipya vya mapato katika Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo yatatolewa katika baraza la madiwani la robo yapili linalotarajiwa kufanyika hivi karibuni kupisha madiwani hao kupitia Mapendekezo hayo na Kisha Kutoa maamuzi yenye tija Kwa Halmashauri hiyo.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...