Na Issa Mwadangala.
Waumini wa Kanisa Katoliki Parokia ya
Mtakatifu Thomas More Jimbo Kuu la Mbeya wametakiwa kuzishinda dhamiri
zao mbaya ili kutotenda matendo uhalifu katika jamii.
Hayo
yalisemwa na Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi wa
Polisi ACP Theopista Mallya, Disemba 17, 2023 wakati aliposhiriki ibada
hiyo ya misa takatifu na kutoa elimu kwa waumini walioshiriki ibada hiyo
kuhusu madhara ya kutekeleza dhamiri mbaya akiwa anasisitiza mahubiri
ya Padre Karolo Kavindi wa Parokia hiyo ambayo inapelekea kufanya
ukatili wa kijinsia na unyanyasaji dhidi ya watoto.
Kamanda
Mallya alisema si jambo jema kwa muumini anayekuja kanisani kumcha Mungu
lakini anatekeleza dhamiri mbaya ambayo inampelekea kufanya ukatili na
vitendo vya uhalifu.
Kamanda Mallya aliongeza kuwa kumcha Mungu
ni kuyatenda yale yote aliyoyaelekeza katika biblia na vitabu vitakatifu
pia kuyaishi ili kutokomeza vitendo viovu katika jamii na hapo tutakuwa
tumeishinda dhamiri mbaya ndani ya mioyo yetu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...