Mkuu wa mkoa wa Dodoma Mhe Rosemary Senyamule Disemba 16 2023 alishiriki zoezi la kufanya usafi wa mazingira na wananchi wa jiji la Dodoma  katika maeneo ya mailimbili,Mipango na Mzakwe.

Akizungumza katika zoezi hilo Mhe. Senyamule ameagiza kwa  kila mwananchi  kuwa na tabia  ya kuchukia uchafu katika mazingira yanayowazunguka ili kuepukana na Magonjwa ya miripuko.

“Kila mtu anahaki ya kutunza mazingira ili kuepuka uchafuzi wa mazingira katika maeneo tofauti tofauti kwa kuwa mlinzi wa mazingira katika kuyatunza.

“Viongozi wetu chini ya Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan wamekuwa vinara namba moja katika  kuhamasisha usafi wa mazingira, vile vile madereva wa  mabasi hakikisheni mnakuwa na kibebea taka katika vyombo vya usafi vinavyopita hapa Dodoma kwa sababa hii ni makao Makuu hivyo hata mazingira yawe na hadhi yake."Amesema Senyamule

Kwa Upande Wake, Katibu Tawala Wilaya ya Dodoma jiji Ndg.Sakina Mbugi amemuhakikishia Mkuu wa Mkoa kusimamia maeneo yote ambayo bado yapo katika hali ya uchafu kuweka  mikakati ili kuhakikisha mazingira yanakuwa katika hali nzuri.



 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...