NA EMMANUEL MBATILO, MICHUZI TV

KLABU ya Mlandege Fc imefanikiwa kuutetea ubingwa wake mara baada ya kuichapa Simba Sc bao 1-0 kwenye fainali ya michuano ya Mapinduzi Cup ambayo ilikuwa inaendelea visiwani Zanzibar.

Katika mchezo huo ambao Simba Sc ilifanikiwa kuutawala mchezo kwenye vipindi vyote licha ya kutofanikiwa kupata bao huku wakiruhusu kufungwa bao moja na kushindwa kunyakua taji hilo.

Bao pekee ambalo limewafanya Mlandege Fc kuibuka washindi limefungwa na Joseph Akandwanao mnamo dakika ya 54 ya mchezo baada ya kuwatoka mabeki wa Simba Sc na kupiga shuti kali lililomshinda kipa na kuingia nyavuni.

Ikumbukwe Mlandege Fc kabla ya fainali haijawahi kushinda ndani ya dakika 90 kwenye michuano hiyo ya kipindi hiki.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...