Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba amekutana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Indonesia Mhe. Pahala Mansury jijini Jakarta, kwa ajili ya kuangalia hatua za mwisho za maandalizi ya Ziara ya Kitaifa ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan itakayofanyika kuanzia tarehe 24-26 Januari, 2024 nchini humo.

Viongozi hao wamekubaliana kuwa maandalizi yote kwa ajili ya ziara hiyo yamekamilika na wako tayari kumpokea Mhe Rais tarehe 24 Januati atakapowasilo nchini Indonesia.

Akizungumza katika kikao hicho Mhe. Waziri Makamba amesema ziara hiyo ni muendelezo wa Jitihada za Serikali ya Awamu ya Sita kayika kukuza na kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia uliopo kati ya Tanzania na Indonesia ambao mwaka huu unatimiza miaka 60 tangu kuanzishwa kwake.

Ameongeza kuwa ziara hiyo pia inalenga kuimarisha Ushirikiano kati ya Tanzania na Indonesia katika maeneo ya kımkakati ya biashara, uwekezaji, Afya, elimu, uchumi wa buluu na kilimo.

Naye Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Indonesia Mhe. Siregar amesema Indonesia iko tayari kumpokea Mhe Rais Samia nchini mwao na kuahidi kuwa Indonesia inauthamini uhusiano wake na Tanzania na itaendela kushirikiana kwa manufaa ya pande zote mbili.

Rais wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwa na ziara ya Kitaifa nchini Indonesia kuanzia tarehe 24-26 Januari 2024.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...