Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya NHIF Bernard Konga akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na Maboresho ya Kitita cha Mafao jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya NHIF Bernard Konga akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na Maboresho ya Kitita cha Mafao jijini Dar es Salaam.

*Kitita cha Mafao chenye maboresho kuanza Machi Mosi

Na Chalila Kibuda,Michuzi TV
MFUKO  wa Taifa wa bima ya Afya NHIF umesema imefanya maboresho ya kitita cha mafao kwa wanachama wake pamoja kuangalia madai yaliyokuwapo kwa madaktari ikiwa ni kutaka wanachama wanapata huduma bora na Mfuko kuwa na uendelevu.

Katika maboresho hayo wanachama watapata huduma za kibingwa bobezi kuanzia ngazi ya Hospitali za kanda.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Bw. Bernard Konga amesema kitita cha mafao ni orodha ya huduma za matibabu ambazo zimetolewa kwa wanufaika na bei zake nchini huku kitita hicho kikabaki vilevile bila kuongeza fedha nyingine .

Amesema maboresho ya mwisho ya kitita cha mafao hayo kimezingatia maoni ya wadau na kuweka milango kuendelea kuboresha lengo ni wanachama wasipate usumbufu.

Hata hivyo amesema kuwa katika maboresho wameongeza ulinzi wa mfuko katika kudhibiti mianya ya udanganyifu juu ya kupata huduma wasio wanachama.

“Ni miaka Nane sasa tangu maboresho ya hiki kitita cha mafao kinachotumika kufanyika hivyo ni muhimu wa kufanya marejeo kutokana na mahitaji ya sasa.

"Umuhimu wa kufanya marejeo kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kuboresha upatikanaji wa huduma bora kwa wanachama na kuongeza huduma ambazo hazikuwepo kwenye kitita cha mafao”,amesema Konga.

Amesema wanachama wanaotumia dawa za shinikizo la damu na sukari sasa wanaweza kupata huduma kuanzia ngazi ya chini huku wanachama wanaopata huduma ya uchujaji damu gharama zikiwa zimepunguzwa.

“Huduma za kibigwa na bingwa bobezi kama matibabu ya Moyo,Saratani na Figo sasa zinaweza kutolewa kuanzia ngazi ya kanda na sio lazima mwanachama kwenda ngazi ya Taifa”,Amesema.

Aidha ameongeza kuwa changamoto ya ukosefu wa dawa sasa imeisha kwani dawa mpya zaidi ya 247 zimeongezwa kwenye kitita kwenye maboresho yaliyofanyika.

Konga amesema maeneo yaliyofanyiwa maboresho ili kuleta unafuu ni gharama za usajili na ushauri wa daktari huduma za dawa na tiba za upasuaji na vipimo huku akisisitiza kuwa gharama za maboresho hayo hazimgusi mwanachama bali kati ya NHIF na mtoa huduma.

Amesema maboresho ya kitita hicho yanatarajia kuanza rasmi Marchi Mosi,2024 huku mfuko huo unaendelea kupokea maoni kutoka kwa wadau kuhusu maboresho zaidi ya kitita hicho.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...