NA EMMANUEL MBATILO, MICHUZI TV

KLABU ya Yanga imeshindwa kutamba kwenye uwanja wake wa nyumbani mara baada ya kulazimishwa sare na Mamelodi Sundowns 0-0.

Katika mchezo huo ambao ulipigwa kwenye dimba la Benjamini Mkapa Jijini Dar es Salaam, Mamelodi waliweza kuutawala mchezo katika kipindi cha kwanza ambapo walitawala kwa asilimia 73% kwa 23% licha ya Yanga Sc kuwa na mashuti matatu yaliyolenga lango huku Mamelodi wakiwa wamepiga moja tu.

Kipindi cha pili Yanga walibadilika na kuonesha hali ya kulitaka bao la kuongoza bila mafanikio licha ya kupata nafasi za wazi nyingi.

Sifa za kipekee zimuendee mlinda mlango wa kimataifa wa Afrika Kusini, Ronwel Williams ambaye aliokoa hatari nyingi ambazo zilitengenezwa na Yanga Sc.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...