Barabara ya Dar es salam-Lindi-Mtwara sasa imerejea katika hali ya kupitika baada ya kukamilika urejeshaji wa mawasiliano katika maeneo yote yaliyokuwa yamekatika.
Mvua kubwa zilizoambata na Kimbunga Hidaya ziliharibu miundombinu ya barabara hiyo katika eneo la Mikereng’ende, Songas, Somanga na Matandu-Nangurukuru ambayo yalikatika kutokana na mvua zilizonyesha na kuambatana na Kimbunga Hidaya.
Juzi tarehe 9 Mei 2024 Magari ya Mizigo, Mabasi na magari mengine madogo yaliyokwama yalianza kuruhusiwa kuendelea na safari jambo ambalo liliamsha hisisa mseto kwa wananchi kuwapongeza wataalamu wa Wizara ya Ujenzi kupitia Wakala ya Barabara (TANROADS) kwa kazi waliyoifanya usiku na mchana katika kurejesha miundombinu hiyo.
Wakati huu wa mvua zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali, wananchi, wasafiri, wasafirishaji na watumiaji wengine wa barabara wanapaswa kusafiri kwa tahadhari kwani maeneo mengine yanaendelea na matengenezo.









Mvua kubwa zilizoambata na Kimbunga Hidaya ziliharibu miundombinu ya barabara hiyo katika eneo la Mikereng’ende, Songas, Somanga na Matandu-Nangurukuru ambayo yalikatika kutokana na mvua zilizonyesha na kuambatana na Kimbunga Hidaya.
Juzi tarehe 9 Mei 2024 Magari ya Mizigo, Mabasi na magari mengine madogo yaliyokwama yalianza kuruhusiwa kuendelea na safari jambo ambalo liliamsha hisisa mseto kwa wananchi kuwapongeza wataalamu wa Wizara ya Ujenzi kupitia Wakala ya Barabara (TANROADS) kwa kazi waliyoifanya usiku na mchana katika kurejesha miundombinu hiyo.
Wakati huu wa mvua zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali, wananchi, wasafiri, wasafirishaji na watumiaji wengine wa barabara wanapaswa kusafiri kwa tahadhari kwani maeneo mengine yanaendelea na matengenezo.










Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...