SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) limeshiriki katika maonesho ya wizara ya viwanda na Biashara katika viwanja vya Bunge yanayoendelea jijini Dodoma.

Wakiongea na maafisa wa TBS baadhi ya waheshimiwa wabunge waliotembelea banda la TBS wameipongeza TBS kwa kazi nzuri wanayofanya ya kuhakikisha usalama na ubora wa bidhaa unazingatiwa ili kumlinda mlaji wa mwisho.

Mkurugenzi Mkuu wa (TBS) , Dkt. Athuman Ngenya amewashukuru Waheshimiwa wabunge kwa kuweza kutenga muda wao kutembelea banda la TBS sambamba na kusikiliza wasilisho kuhusu majukumu ya Shirika na utekelezaji wake na kuahidi kutekeleza maelekezo yote waliyopewa kwa manufaa ya wananchi.

Maonesho hayo yamelenga kuwapatia fursa waheshimiwa wabunge kuongeza uelewa juu ya shughuli zinazofanywa na taasisi zilizopo chini ya Wizara ya Viwanda na Biashara.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...