Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) Evans Nyangasa akizungumza Mkurugenzi wa Bodi ya Mkonge Tanzania Saady Kambona na Meneja wa Tarura Mkoa wa Tanga kulia wakati walipotembelea banda lao katika viwanja vya Usagara Jijini Tanga kunakoendelea maonyesho ya Biashara na Utalii

Na Oscar Assenga, TANGA
MFUKO wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoa wa Tanga katika zoezi la uhakiki wa wanachama kwenye vituo vya kutolea huduma umebaini uwepo wa wanachama zaidi ya 130 ambao sio halali

Hayo yalibainishwa na Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Mkoa wa Tanga Evans Nyangasa wakati akizungumza na waandishi wa habari katika maonyesho ya biashara na utalii yanayoendelea kwenye viwanja vya shule ya Sekondari Usagara Jijini humo

Alisema uhakiki huo ulifanyika kati ya mwezi June 2023 mpaka sasa na katika udanganyifu huo kuna baadhi ya waliotumia huduma hizo wameweza kuzilipia gharama ambazo walitumia ndivyo sivyo huku wakitoa wito kwa watoa huduma kutoa kwa mwanachama sahihi na kwa wakati sahihi na huduma halali.

“Kwa kwa wakati sahihji mna huduma halali na wamejipanga kutoa huduma kwa wananchi kwenye nyumba za ibada,mashule na vijiji ili waweze kujiunga na bima ya afya lengo lao ni kuhakikisha kila mwananchi anajiunga na mfuko huo"Alisema

Alisema lengo lao ni kuhakikisha wanaendelea kutoa elimu juu ya matumizi mazuri ya kadi ya bima ya afya kutokana na kwamba siku za karibuni kumeibuka miongoni mwa wanachama wanashiriki udanganyifu kutumia kadi zao ndio sivyo jambo ambalo linapelekea mfuko kutumia gharama nyingi.

“Tunaendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhakikisha wanatumia kazi zao vizuri wanapokwenda kwenye vituo vya kutolea huduma ndio maana Tanga tumejipanga kuendelea kuweka watalaamu kwenye vituo vya kutolea huduma kwa lengo la kudhibiti udanganyifu ambao unaweza kutokea wakati wa utoaji wa huduma na nisisitize wananchi waendelea kuzingatia miongoozo na taratibu za huduma”Alisema

Hata hivyo alisema wameamua kushiriki kwenye maonyesho hayo kwa lengo la kutoa elimu kwa watanzania juu ya huduma zinazotolewa ikiwemo umuhimu wa kuwa na bima ya afya kwa wananchi kutokana na kwamba inawapa uhakika wa kugharamia gharamaza za matibabu bila kulipia gharama za ziada.

“Pamoja na kutoa elimu lakini pia tunapokea malalamiko na maoni kutoka kwa wanachama wetu juu ya huduma zinazotolewa na mfuko na kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu na kuwa na huduma bora kwa wanachama wa pale wanaponufaika na huduma hizo”Alisema



Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) Evans Nyangasa akizungumza Mkurugenzi wa Bodi ya Mkonge Tanzania Saady Kambona na Meneja wa Tarura Mkoa wa Tanga kulia wakati walipotembelea banda lao katika viwanja vya Usagara Jijini Tanga kunakoendelea maonyesho ya Biashara na Utalii


Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Tanga Shymaa Kwegyir kulia akipatiwa huduma kwenye Banda la NHIF

MKUU wa Mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian kulia akisalimiana na Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) Evans Nyangasa wakati alipokwenda kufungua maonyesho ya biashara na utalii yanayoendelea kwenye viwanja vya Usagara Jijini Tanga

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...