Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Dkt. Selemani Jafo ameshiriki zoezi la Uandikishaji kwenye Daftari la Wapiga kura kwa ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa katika Kitongoji cha Kimani wilaya ya Kisarawe Mkoani Pwani leo Oktoba 12,2024.

Na.Alex Sonna-KISARAWE

Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Dkt. Selemani Jafo ameshiriki zoezi la Uandikishaji kwenye Daftari la Wapiga kura kwa ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa katika Kitongoji cha Kimani wilaya ya Kisarawe Mkoani Pwani.

Akizungumza leo Oktoba 12,2024 mara baada ya kujiandikisha Mhe.Dk.Jafo amewahimiza wananchi wa Kisarawe kujitokeza kwa wingi na kujiandikisha katika vituo vya kujiandikisha wapiga kura ili waweze kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika Novemba 27, 2024.

Dk.Jafo amesema zoezi la kujiandikisha katika daftari la kupiga kura ni muhimu kwa kuwa ni wajibu kushiriki katika kuchagua viongozi watakaoweza kuwasaidia wananchi.

"Viongozi wa serikali za mitaa ndiyo wanaoishi jirani zaidi na wananchi hivyo ni muhimu kushiriki katika kuwachagua wale watakaolinda maslahi ya jamii husika."amesema Dk.Jafo
Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Dkt. Selemani Jafo ameshiriki zoezi la Uandikishaji kwenye Daftari la Wapiga kura kwa ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa katika Kitongoji cha Kimani wilaya ya Kisarawe Mkoani Pwani leo Oktoba 12,2024.
Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Dkt. Selemani Jafo, akijiandikisha kwenye Daftari la Wapiga kura kwa ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa katika Kitongoji cha Kimani wilaya ya Kisarawe Mkoani Pwani leo Oktoba 12,2024.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...