Na Beatus Maganja, Mbeya.

Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania - TAWA imekutana leo Machi 18, 2025 Jijini Mbeya Kwa ajili ya kuanza kikao chake cha Kawaida cha 30 cha Bodi hiyo inayoongozwa na Mwenyekiti wake Meja  Jenerali (Mstaafu) Hamis R. Semfuko.

Katika kikao cha siku ya Kwanza (Leo) wajumbe wa kamati za Sera, Mipango na Fedha inayoongozwa na Dr. Simon Mduma na kamati ya Ulinzi wa Rasilimali ya Wanyamapori na Uendeshaji na Usimamizi wa Rasilimali watu inayoongozwa na Prof. Jafari Kideghesho wamekutana  na kujadili masuala mbalimbali yanayohusu Maendeleo na ustawi wa Taasisi hiyo.

Aidha kikao hicho kinatarajiwa kufanyika Kwa siku nne ambapo Bodi itapata fursa ya kutembelea Hifadhi ya Mpanga/Kipengere na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo miundombinu ya utalii, miradi inayotekelezwa na TAWA hifadhini humo.







Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...