Na John Mapepele -Moshi

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais- TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa leo amekagua uharibifu wa barabara ya Spencon- Fongagate- Mabogini- Chekereni hadi Kahe yenye urefu wa kilomita 31.25 na kuiagiza Wakala ya Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA) kuanza mara moja kujenga kwa kiwango cha lami.

Akizungumza kwa nyakati tofauti na wananchi wa Mabogini na Kahe amesema Serikali inakwenda kujenga kwa kiwango cha lami Ili ipitike katika kipindi chote cha mwaka ikiwa ni utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi.
Aidha, amesema kukamilika kwa barabara hiyo kutarahisisha huduma ya usafiri kwa wananchi kwenda kupata huduma ya afya na elimu.

" Kukamilika kwa barabara hii kutasaidia wananchi wetu kufikisha mazao yao sokoni kwa maana ya Moshi Mjini na maeneo mbalimbali nchini hivyo kukuza kilimo cha mazao ya mpunga, mahindi na miwa ambayo yameonyesha kusitawi vema kwenye eneo hili" . Amefafanua Mhe. Mchengerwa 
Amesema katika awamu ya kwanza ya ujenzi wa barabara hiyo utahusisha ujenzi wa mitaro mikubwa kwa pande zote mbili, madaraja na kuweka mawe na kifusi ambapo utaifanye ipitike katika misimu yote ya mwaka.

Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa TARURA, Mhandisi Victor Seiff amesema mradi wa ujenzi wa barabara hiyo hadi kukamilika kutagharimu takribani bilioni 45 ambapo awamu ya kwanza itagharimu jumla ya shilingi bilioni 7.



Pia Waziri Mchengerwa amezielekeza Halmashauri zote nchini kukusanya mapato ya ndani na kuanza kutenga 10% kwa ajili ya ujenzi wa barabara.

Wakati huohuo amewaagiza wakuu wote wa mikoa na Wilaya kuendelea kulinda amani na kudhibiti vitendo vyovyote vinavyoweza kusababisha uvunjifu wa amani.

Next
This is the most recent post.
Previous
Older Post

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...