Tarehe 5 Mei 2025 Historia imeandikwa.
NI rasmi kwamba Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni mmiliki wa teknolojia ya uzalishaji wa viuadudu (biolarvicides), viuatilifu hali (bio pesticides) na mbolea hai (bio fertilizer)
Shukrani za dhati kwa Mhe. Rais Mama Samia Suluhu Hassan na Serikali kwa ujumla kwa kuliwezesha hili kwa manufaa ya watanzania.
Sasa tunaweza kuongea kwa kujiamini kwamba ule mwisho wa ugonjwa wa malaria umefika. Sasa tunaweza kuongea kwa kujiamini kwamba tutazalisha mazao yetu pasina kutumia viuatifu na mbolea zenye sumu na zenye madhara kwa binadamu. Huu ni ushindi kwetu sote!
Hii ndio tafsiri sahihi ya Uhuru wa Nchi na Taifa, Utoshelevu wa kimaarifa, kiujuzi, kiubinifu, kiteknolojia, Ujamaa na Kujitegemea.
Mungu Ibariki Tanzania
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...