NA WILLIUM PAUL, MOSHI

KATA ya Mabogini imepokea kiasi cha shilingi bilioni 1.8 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya. 

Hospitali hii ni ya wakazi wa Halmashauri ya Moshi ambayo imejengwa kwa lengo la kuboresha huduma za afya na kuzisogeza karibu na wananchi. 

Hospitali hiyo ambayo bado haijakamilika, imeshaanza kutoa huduma ambapo Majengo yaliyokamilika ni jengo la wagonjwa wa nje (OPD), Maabara, Jengo la Mama na Mtoto, Jengo la Kufulia, Stoo ya Madawa na Jengo la Utawala.

Hospitali hii itakuwa ni msaada mkubwa kwa wananchi wa maeneo ya tambarare inayobeba Kata za Mabogini, Arusha Chini, Maeneo ya Tambarare ya Kata za Oldmoshi Magharibi,  na Kimochi, Kahe Magharibi na Kahe Mashariki.

Hospitali hii imepatikana kwa juhudi za Mbunge wa Jimbo la Moshi Vijijini  Profesa Patrick Ndakidemi na Diwani wa Kata ya Mabogini  Dkt. Bibiana Massawe. 




 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...