RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ametoa mkono wa pole kwa familia ya marehemu Charles Hillary, aliyekuwa Msemaji Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, aliyefariki dunia usiku wa kuamkia leo, tarehe 11 Mei 2025, jijini Dar es Salaam.

Rais Dkt. Mwinyi amefika nyumbani kwa marehemu, Mtaa wa Kibamba CCM, Wilaya ya Ubungo, jijini Dar es Salaam, kutoa mkono wa pole kwa mjane wa marehemu, Bi Sarah Mwakanjuki, pamoja na wanafamilia, ndugu, jamaa na marafiki.

Rais Dkt. Mwinyi amewataka wote walioguswa na msiba huo kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha majonzi.

Marehemu Charles Hillary amefariki akiwa na umri wa miaka 66.

Rais Dkt. Mwinyi alimteua kuwa Mkurugenzi wa Idara ya Mawasiliano Ikulu tarehe 30 Desemba 2021, na baadaye akamteua tena kuwa Msemaji Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar tarehe 6 Februari 2023.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...