Na Janeth Raphael MichuziTv- Bungeni -Dodoma
WIZARA ya Elimu,Sayansi na Teknolojia inajivunia kuunganisha mifumo ya takwimu za elimu na kuwa na mfumo mmoja wa sekta ya elimu.
Hayo yameelezwa leo Mei 12,2025 bungeni na Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia,Profesa Adolf Mkenda wakati akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2025-2026.
Waziri Mkenda amesema takwimu za elimu ni nyenzo muhimu katika kuboresha ufundishaji na ujifunzaji, kufanya tafiti na kutoa maamuzi mbalimbali.
"Kwa kutambua umuhimu huo, Serikali imeunganisha mifumo ya takwimu za elimu na kuwa na mfumo mmoja wa sekta ya elimu,"amesema Waziri Mkenda
Aidha,Wizara imeendelea na ujenzi wa Mfumo wa Takwimu wa Sekta ya Elimu utakaowezesha upatikanaji wa takwimu zote za sekta kupitia mfumo huo.
Aidha, mfumo huo utakuwa na uwezo wa kupokea takwimu mbalimbali zinazohusiana na elimu kutoka katika mifumo mingine ya Serikali ikiwemo NIDA, RITA, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Idara ya Uhamiaji na OR–TAMISEMI.

WIZARA ya Elimu,Sayansi na Teknolojia inajivunia kuunganisha mifumo ya takwimu za elimu na kuwa na mfumo mmoja wa sekta ya elimu.
Hayo yameelezwa leo Mei 12,2025 bungeni na Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia,Profesa Adolf Mkenda wakati akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2025-2026.
Waziri Mkenda amesema takwimu za elimu ni nyenzo muhimu katika kuboresha ufundishaji na ujifunzaji, kufanya tafiti na kutoa maamuzi mbalimbali.
"Kwa kutambua umuhimu huo, Serikali imeunganisha mifumo ya takwimu za elimu na kuwa na mfumo mmoja wa sekta ya elimu,"amesema Waziri Mkenda
Aidha,Wizara imeendelea na ujenzi wa Mfumo wa Takwimu wa Sekta ya Elimu utakaowezesha upatikanaji wa takwimu zote za sekta kupitia mfumo huo.
Aidha, mfumo huo utakuwa na uwezo wa kupokea takwimu mbalimbali zinazohusiana na elimu kutoka katika mifumo mingine ya Serikali ikiwemo NIDA, RITA, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Idara ya Uhamiaji na OR–TAMISEMI.

Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...