Na Oscar Assenga, Tanga

Tanga Yetu kupitia mradi wa Fursa kwa Vijana (GOYN TANGA ) kwa kushirikiana na Bodi ya Filamu Tanzania wametoa mafunzo kwa ajili ya utengenezaji wa filamu kwa wasanii mkoani Tanga ili waweze kuwa waandaaji wazuri ambao watafanya vizuri kupitia tasnia hiyo.

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo Afisa Maendeleo ya Filamu kutoka Bodi ya Filamu Tanzania Ally Makata kwa niaba ya Serikali alisema kwamba wamekuja Tanga mara ya pili kutoa mafunzo kuhusu utengenezaji wa filamu kwa wasanii wa filamu mkoani Tanga.

Alisema kwamba mafunzo hayo waliyatoa kwa awamu tatu ambapo ya kwanza ilikuwa ni watu wakwenda kufanya utafiti watu wapate wazo kwamba endapo watapata muongozo nani anaweza kucheza na bajeti ya kiasi gani na nani anaweza kufadhili ikiwemo kutengeneza hadithi fupi fupi lazima mdau yoyote kwenye filamu aweza kufanya hivyo ili aweze kufanya vizuri.

Aidha alisema kwamba baada ya hapo awamu ya pili na tatu ni kushika Kamera kuona namna kutengeneza mwanga na watu kwenda kwenye maeneo husika na uhariri pamoja na namna ya kupanga na kutengeneza sauti ili uweza kupata picha kamili na viti vyengine.

“Tunawashukuru Tanga Yetu kwa kuweza kufadhili na kushirikiana na Bodi ya Filamu nchini kwa watayarishaji wa Mkoa wa Tanga waweze kupata maarifa kutokana na kwamba Tanga kwa asilimia kubwa  ipo chini na watayarishaji wa Tanga wanalalamika kwenye media wanaoka kazi za mikoa mengine na ikitokea tuzo mikoa mwengine inashika tuzo”Alisema

“Wakati ukiangalia Tanga kuna rasimali za kila kitu ukiangalia mandhara wana sehemu za vivutio wana mazingira mazuri tamaduni wana vyakula tamaduni watu wanaishi kila siku kwanini tusipate Filamu inayoakisi Jamii ya Mkoa wa Tanga “Alisema

Alisema kwamba ukiangalia Marehemu King Majuto ameshaandoka ambaye alikuwa anaiwakilisha vizuri mkoa wa Tanga ikiwemo Marehemu Bauji tunapata stori kulikuwa na waandishi wazuri na waigizaji wazuri lakini sasa haifanyiki hivyo shabaha kubwa ya Dkt Omari na Taasisi ya Tanga Yetu ni kuona namna Tanga inarudi upya.

 Aliongeza kwamba ukiachana na hayo mafunzo wanaandaa mpango mkakati wa kuona mtayarishaji wa Tanga endapo ataomba Fedha DW na Taasisi mbalimbali ataulizwa historia ya sehemu alipo sasa wakipata mpango mkakati itakuwa rahisi watayarishaji wa mkoa wa Tanga kuchukua mpango mkakati na kuandaa kila wanachokiandaa na kwenda kuombea fedha.

 

Alisema wanawapatia mafunzo na maarifa ili kesho na kesho kutwa waweze kufanya vizuri mkoa wa Tanga ili waweze kufanya vziuri na kurejesha katika hali yake ya kawaida na kung’ara vziuri.

 Awali akizungumza Mkurugenzi wa HD Consalt Omari Bakari ambao wanatekeleza mradi wa Fursa kwa vijana wa Tanga (GOYN) kupitia program ya Tanga Yetu alisema lengo kubwa ni kuhakikisha vijana wa Jiji la Tanga wanapata fursa ya kuajiriwa au kujiajiri wenyewe.

 Alisema uchambuzi ambao waliifanya na ofisi ya Taifa ya Takwimu vijana walionekana kutokuea na mahotaji sawa kutokana kila mmoja na uwezo wake na chaguo lake mpango huo wanaoshirikiana na Bodi ya Filamu ni inalenga kusaidia kufikia lengo kwa vijana wale ambao walisema wanapenda kuwa kwenye filamu.

Alisema waliamua kushirikiana na Bodi ya Filamu kama Taasisi ya Serikali waliamini kama wana majukumu ya kusimamia,kuhamasisha na kutangaza hiyo sekta kwa hiyo walikubaliana  kuendelea na kusaidia hayo mafunzo yaliyoanza kwenye uzalishaji na wazo kubwa ni kuhakikisha vijana wanapata uzoefu kwenye sekta binafasi ambazo zinashirikiana na bodi ya filamu.

“Leo imefikia mwisho wa awamu ya pili na tutaenda kwenye awamu ya tatu kuzalisha filamu ambazo zitakwenda kwenye soko hivyo niwaombe wadau mbalimbali hao vijana wapo vizuri ni kuwaamini na kuwapa kazi ambazo wanaweza kufanya nao wataweza kuwasaidia”Alisema


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...