OR- TAMISEMI
Naibu Waziri Ofisi ya Rais – TAMISEMI Mhe. Zainab Katimba amesema serikali itaendelea kusimamia Halmashauri zote nchini ili ziweze kutimiza majukumu ya msingi ya kutumia mapato ya ndani ya Halmashauri kwa ajili ya kuimarisha sekta mbalimbali ikiwemo sekta ya Elimu.
Mhe. Katimba amesema hayo leo bungeni jijini Dodoma kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI Mhe. Mohamed Mchengerwa wakati akijibu swali la Mhe. Mwita Waitara, Mbunge wa Tarime Vijijini aliyeitaka Ofisi ya Rais – TAMISEMI kutoa muongozo kwa Halmashauri kwa mwaka wa fedha ujao ili kila Halmashauri iweke mpango wa kumaliza tatizo la meza, viti na madawati.
Akijibu swali hilo Mhe. Katimba amesema “Nitumie nafasi hii kuendelea kutoa msisitizo kwa wakurugenzi wetu wa Halmashauri zote 184 waweze kutimiza wajibu wao wa msingi wa kutenga fedha kutoka kwenye mapato ya ndani na kuweza kuziweka kwenye mipango na bajeti kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo” amesema
Katika hatua nyingine Mhe. Katimba amesema kwa mwaka wa fedha 2025/26 serikali inatarajia kutumia kiasi cha shilingi bilioni 613 pamoja na mapato ya ndani ya Halmashauri ili kutekeleza shughuli mbalimbali za maendeleo ikiwemo upatikanaji wa madawati.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...