Kada wa Chama Cha Mapinduzi CCM, Abuubakari Ally ( Boka) amechukua fomu ya kuomba ridhaa ya kuteuliwa kugombea nafasi ya Ubunge katika Jimbo la Kigamboni, Dar es Salaam.
Abuubakari, ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati ya Siasa Mkoa wa Dar es salaam, amefika katika ofisi za Chama wilayani humo leo na kukabidhiwa fomu na Katibu wa CCM wa wilaya hiyo, stanley Mkandawile.
Pamoja na kujihusisha na Siasa Boka ni mdau wa masuala ya afya na michezo nchini.
Wengine waliochukua fomu katika jimbo hilo ni Ally Mandai, Rais wa Yanga Mhandisi Hersi Said, Dokta Henjewele,Diwani wa Kata ya Msasani Luca Nighest.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...