Na MWANDISHI WETU
DIWANI wa Kata ya Marumbo, Kisarawe, mkoani Pwani, Msafiri Mpendu, amemshukuru Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, kwa kuifungua kata hiyo kupitia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika kipindi cha miaka mitano.
Ameyasema hayo alipowasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya Kata ya hiyo kwa mwaka wa fedha 2020 -2025 .
Diwani Mpendu, amesema zaidi ya sh. milioni 227 zimepelekwa katika sekta ya afya kwenye miradi ya ujenzi wa zahanati, nyumba za watumishi na usambazaji wa mifumo ya maji.
Ameeleza, a katika sekta ya elimu sh. milioni 239 zilipokelewa na kuelekezwa fedha katika maendeleo ya miundombinu ya elimu kama ujenzi wa madarasa, vyoo,majiko na ugawaji magodoro kwa wanafunzi.
Akizungumzia sekta ya maji katika kata hiyo, Mpendu amesema wananchi wamenufaika na uchimbaji wa visima 16 vilivyochimbwa kimkakati.
“Lengo ni kuhakikisha visima hivi vinahudumia idadi kubwa ya watu katika vijiji vyote vya kata hii ya Marumbo, kazi iliyofanywa na serikali pamoja na wadau,”amesema.
Kuhusu miundombinu ya barabara, Mpendu, amebainisha ibainisha uboreshaji huo umechochea kiuchumi na kurahisisha upatikanajiwa huduma za kijamii.
Ameushukuru Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (TARURA) kuhakikisha barabara muhimu zinapitika kwa urahisi katika misimu yote ya mwaka.
Kuhusu huduma za kijamii Diwani Mpendu, amesema hatua zinaendelea kuchukuliwa katika mpango wa kuimarisha lishe ambapo katika kipindi cha miaka mitano jumla ya ng'ombe 1400 walichinjwa.
“Tuligawa nyama kwa wananchi. Pia tuligawa vyakula mbalimbali katika familia zenye mahitaji maalumu kusaidia lishe hasa kwa watoto,”amesema.
Amesema uwezeshaji huo ulifanywa ni diwani kwa kushirikiana na wafadhili..
Mpendu alisema katika kuinua wanawake,vijana na watu wenye ulemavu kiuchumi, serikali chini ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan ilitoa kiasi cha sh. milioni 25 ambapo vikundi vinne katika kata hiyo vimepata mikopo ya kuanzisha na kukuza biashara.
“Kero ya mawasiliano katika kata hii imepatiwa ufumbuzi kwa kuwekwa minara miwili ya kampuni za simu hali iliyorahisisha mawasiliano na kufungua fursa ya kukuza uchumi, kurahisisha huduma za kutuma na kupokea fedha tofauti na awali,”ameeleza Diwani Mpendu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...