Kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kulwa Biteko kwa mara nyingine amechukua fomu ya kugombea ubunge katika Jimbo jipya la Katoro lililopo katika mamlaka ya mji mdogo wa Katoro wilayani Geita.

Hii ikiwa ni muendelezo wa harakati zake kisiasa,ambapo mnamo mwaka 2020 alichukua fomu ya kugombea jimbo hilo ambalo hapo kabla liliitwa jimbo la Busanda.

Jimbo la katoro lilipatikana baada ya mchakato wa kugawa majimbo ulipokamilika na kupata majimbo mawili yaani jimbo la Katoro na Jimbo la Busanda.

Katibu wa Chama Cha Mapinduzi wilaya ya Geita Michael Msuya amesema kuwa dirisha la uchukuaji wa fomu za ubunge na udiwani limefunguliwa rasmi leo tarehe 28 kuanzia saa mbili asubuhi mpaka saa 10 jioni.

Amewasihi watia nia kufata kanuni za chama kutoleta mbwembwe wakati wa uchukuaji wa fomu hizo ili kuondoa vurugu ambazo hazina msingi.






Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...