Mbunge wa jimbo la Ngara Mhe. Ndaisaba George Ruhoro amechukua fomu ya maombi ya kugombea tena nafasi ya ubunge kwa kipindi kingine cha 2025/30 kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Fomu hiyo ameichukua leo Juni 30 2025 katika Ofisi za Chama Cha Mapinduzi CCM Ngara Mkoani Kagera.

Hata hivyo vyombo vya habari vilivyokuwepo katika eneo la tukio walipotaka mahojiano hakuwa tayari kuzungumzia chochote zaidi alisema wakati ukifika atazungumza.

Ikumbukwe kuwa Mheshimiwa Ruhoro ni miongoni mwa viongozi wenye ushawishi mkubwa kwa wananchi wa jimbo lake kwani wananchi hao wamekuwa wakimchangia fedha kwa ajili ya kuchukua fomu ya kugombea tena katika kipindi kingine 2025-2030.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...