Stanbic Bank Tanzania leo imewazawadia wateja 32 waliobahatika katika droo ya kwanza ya kampeni yake ya Salary Switch, ambapo walishinda zawadi mbalimbali za fedha taslimu hadi kufikia TZS 500,000. Droo hii imefanyika ikiwa ni mwezi mmoja tangu kuzinduliwa rasmi kwa kampeni hiyo inayolenga kuhamasisha wafanyakazi kuhamishia akaunti zao za mshahara Stanbic Bank.

Tukio hilo limefanyika katika makao makuu ya benki jijini Dar es Salaam na limeshuhudiwa rasmi na Bi. Irene Kawili, mwakilishi kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, pamoja na wanahabari – kuhakikisha uwazi na uadilifu katika mchakato huo.

Akizungumza wakati wa tukio hilo, Priscus Kavishe, Meneja Mwandamizi – alisema “Tumefurahishwa sana na mwitikio mkubwa kutoka kwa wateja kote nchini. Droo hii ya kwanza ni njia yetu ya kushukuru kwa imani yao. Kwa kuhamishia mshahara wao Stanbic, wateja wetu wanapata zaidi ya huduma za kawaida – wanapata fursa halisi zenye thamani.”

Kampeni ya Salary Switch inatoa faida mbalimbali kwa wateja wanaoshiriki, ikiwemo fursa ya kupata mkopo wa mshahara hadi 60%, bima ya msiba bure kwa familia, ushauri wa kifedha wa binafsi kupitia programu ya Financial Fitness Academy, pamoja na nafasi ya kushinda zawadi za pesa taslimu kila mwezi.

Washindi 32 waliotangazwa leo wametoka katika maeneo mbalimbali ya Tanzania na walichaguliwa kwa bahati nasibu kutoka kwa waliotimiza masharti ya ushiriki kwa mwezi uliopita.

Shabani Mwenda, Kaimu Mkuu wa Idara ya Ugeuzi wa Huduma kwa wateja, aliongeza:

“Tumejikita kutoa thamani zaidi ya huduma za kifedha. Salary Switch si kampeni tu – ni ahadi yetu kwa wateja kuwa tupo pamoja nao katika safari yao ya kifedha, kila hatua ya njia.”

Kampeni ya Salary Switch inaendelea katika matawi yote ya Stanbic Bank nchini, ambapo droo zaidi na zawadi za kuvutia zitaendelea kutolewa katika miezi ijayo.

Meneja Mwandamizi wa Mauzo Benki ya Stanbic  Tanzania, Priscus Kavishe (katikati) akiwa na Sarah Odunga (kushoto), Meneja wa Thamani kwa Wateja na Irene Kawili (kulia), mwakilishi kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, wakati wa uzinduzi wa droo ya kwanza ya  kampeni ya Salary Switch kwa waandishi wa habari  ambapo washindi 32 walizawadiwa fedha taslimu hadi TZS 500,000

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...