
Na John Mapepele
Mara baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwaapisha na kutoa maelekezo kwa viongozi kadhaa aliowateua ikiwa ni pamoja na Wakuu wa Mikoa, Waziri wa TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa amekutana na kuwafunda.
Mhe. Mchengerwa amewataka kuzingatia maelekezo yote waliyopatiwa na Mhe. Rais huku akisisitiza kuwa wanatakiwa kuwatumikia wananchi kwa kuwa Serikali ni ya wananchi na wasisite kuwasiliana na Wizara wapatapo changamoto.

"Ndugu zangu nadhani mmeiona dhamira ya Mhe. Rais ya kuwataka kwenda kuwatumikia wananchi.Mimi siwezi kuongeza chochote nawaombeni mkayazingatie yale yote aliyowaelekeza" amesisitiza Mhe Mchengerwa
Katika hotuba yake baada ya kuwaapisha Wakuu wa Mikoa hao wapya Mhe. Rais ametoa maelekezo mahususi manne ikiwa ni pamoja na kuwataka kutunza amani na usalama wa wananchi katika mikoa yao kwa kuzingatia kuwa Tanzania inakwenda kwenye uchaguzi mkuu Oktoba mwaka huu.

Aidha amesisitiza kufanya usimamizi madhubuti wa fedha za Serikali ili zitumike kwa kuzingatia thamani ya huduma au bidhaa zinazonunuliwa.
Pia amewaagiza kuhakikisha Wakuu wote wa Mikoa nchini wanasimamiĆ ukusanyaji wa mapato ya ndani bila kutumia nguvu.

Aidha ameelekeka kwenda kuwasikiliza wananchi na kusimama katikati yao huku akisisitiza kujishusha kwa wananchi.
"Kuna fedha nyingi lakini mara nyingi uongozi wa wananchi unafikiria kuwekeza katika vitu vingine badala ya kuwekeza katika mahitaji ya wananchi.Mathalan katika baadhi Halmashauri miundombinu mibovu lakini fedha inayopatikana inawekezwa katika biashara nyingine hiyo siyo sawa". Amefafanua Mhe Rais

Mkuu Mpya wa Mkoa wa Kigoma akitoa neno la shukrani kwa niaba ya wakuu wa mikoa wapya katika kikao na Waziri Mchengerwa aliyeambatana na Katibu Mkuu wa TAMISEMI, Adolf Ndunguru na Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia TAMISEMI amesema wanakwenda kusimamia maelekezo yote yaliyotolewa na Mhe. Rais na kushirikiana na Wizara mama ya TAMISEMI ili kuwatumikia wananchi na kuboresha maisha yao.
Katika kikao hicho Waziri Mchengewa alitoa nyaraka muhimu kwa kila Mkuu wa Mkoa ikiwa ni nyenzo za kazi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...