Dodoma, Tanzania
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene, ametembelea banda la Benki ya NMB katika ufunguzi rasmi wa maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea kufanyika Jijini Dodoma.
Katika ziara hiyo, Mhe. Simbachawene alipata maelezo kutoka kwa Mkuu wa Biashara ya Serikali wa Benki ya NMB, Bi. Vicky Bishubo, kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa na benki hiyo kwa taasisi za umma, ikiwa ni sehemu ya mchango wa NMB katika kuboresha huduma za kifedha na maendeleo ya kiuchumi nchini.
Maadhimisho ya mwaka huu yamewaleta pamoja Wizara, Sekretarieti za Mikoa na Taasisi mbalimbali za Umma, ambapo wanatoa elimu kwa wananchi kuhusu utekelezaji wa majukumu yao, sambamba na kuonesha huduma na bidhaa zinazotolewa kwa manufaa ya umma.
Siku ya Utumishi wa Umma Barani Afrika huadhimishwa kila mwaka tarehe 23 Juni na nchi wanachama wa Umoja wa Afrika (AU), ikiwa ni ishara ya kutambua mchango muhimu wa watumishi wa umma katika maendeleo ya nchi zao na bara kwa ujumla.
Benki ya NMB imekuwa mshiriki hai katika maadhimisho haya kwa kutoa elimu ya kifedha na kuonesha masuluhisho mbalimbali ya kidijitali yanayolenga kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma kwa Watanzania.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene, ametembelea banda la Benki ya NMB katika ufunguzi rasmi wa maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea kufanyika Jijini Dodoma.
Katika ziara hiyo, Mhe. Simbachawene alipata maelezo kutoka kwa Mkuu wa Biashara ya Serikali wa Benki ya NMB, Bi. Vicky Bishubo, kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa na benki hiyo kwa taasisi za umma, ikiwa ni sehemu ya mchango wa NMB katika kuboresha huduma za kifedha na maendeleo ya kiuchumi nchini.
Maadhimisho ya mwaka huu yamewaleta pamoja Wizara, Sekretarieti za Mikoa na Taasisi mbalimbali za Umma, ambapo wanatoa elimu kwa wananchi kuhusu utekelezaji wa majukumu yao, sambamba na kuonesha huduma na bidhaa zinazotolewa kwa manufaa ya umma.
Siku ya Utumishi wa Umma Barani Afrika huadhimishwa kila mwaka tarehe 23 Juni na nchi wanachama wa Umoja wa Afrika (AU), ikiwa ni ishara ya kutambua mchango muhimu wa watumishi wa umma katika maendeleo ya nchi zao na bara kwa ujumla.
Benki ya NMB imekuwa mshiriki hai katika maadhimisho haya kwa kutoa elimu ya kifedha na kuonesha masuluhisho mbalimbali ya kidijitali yanayolenga kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma kwa Watanzania.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...