WATUMIAJI wa bidhaa watakiwa kusoma maelezo yanayopatikana katika vifungashio vya bidhaa kabla ya kununua bidhaa husika hususani muda wa matumizi.

Ushauri huo umetolewa na Afisa Udhibiti ubora wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS) Bi. Sarah Maro, wakati akizungumza na watembeleaji kwenye Maonesho ya Maadhimisho ya Wiki ya Maziwa yaliyofanyika katika viwanja vya zimoto Manispaa ya Morogoro

Alisema watumiaji wa bidhaa wanatakiwa kusoma kwa makini taarifa zilizopo kwenye vifungashio ili kuepuka kununua bidhaa zilizoisha muda wa matumizi.

"Ni muhimu wananchi wakajenga utamaduni wa kusoma taarifa hizo ili kujiridhisha kama zinakidhi matakwa ya viwango ili kuepuka gharama au hasara inayoweza kujitokeza kwa kutumia bidhaa ambazo hazijathibitishwa ubora wake," alisema Maro.

Alisema watu wanaponunua bidhaa baada ya kusoma maelezo wanakuwa na uhakika na bidhaa walizonunua hivyo kuepuka hasara ambazo zingejitokeza kwa kununua bidhaa zisizokidhi mahitaji yao hivyo kuwa salama zaidi kiuchumi pamoja na kiafya

Pamoja na hayo, Maro aliwasisitiza watumiaji wa bidhaa kutoa taarifa endapo watakutana na bidhaa zisizo na viwango au zilizoisha muda wa matumizi kwa lengo la kudhibiti bidhaa hizo kutumika.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...