Na Oscar Assenga,TANGA

WANANCHI wanaoishi kwenye maeneo yanayostahimili kilimo cha Pamba wametakiwa kuchangamkia fursa ya kulima zao hilo ambalo ni la kimkakati la kibiashara kutokana na kwamba linaweza kusaidia kupunguza kiasi cha umaskini kwenye ngazi ya kaya,wilaya na Taifa kwa ujumla

Hayo yalisemwa jana na Afisa wa Bodi ya Pamba Tanzania Alphonce Ngawagala wakati akizungumza na waandishi wa habari katika maonyesho ya 12 ya Biashara na Utalii yanayoendelea kwenye viwanja vya Mwahako Jijini Tanga.

Alisema kwamba lengo la wao kushiriki kwenye maonyesho hayo ni kutangaza fursa zinazopatikana kwenye bodi hiyo kwa kuwaelimisha wananchi maeneo gani yanafaa kulima pamba na pembejeo zinapatikana kwa utaratibu upi ambao ni bure.

Alisema kwamba pia baada ya mkulima na kuvuna wanaanzisha soko la mkulima ili aweze kuuza mazao yake kwa wakati ili aongeze kipato chake apate awekeze kwenye mambo mengine ya kimaendeleo.

Aidha alisema kwamba bodi hiyo imepewa dhamana ya kusimamia usindikaji,uzalishaji na kusimamia masoko pamoja na kuelimisha wananchi maeneo yanayotakiwa kulimwa pamba na pembejeo zinapatikana kwa utararibu upi ambao ni bure na baadae ya kulima hizo wao wanasimamia soko ili wakulima wauze.

“Lakini uchakataji wa Pamba inapokwenda kiwandani napo bodi ipo kwa ajili ya kusimamia inasimamia kuhakikisha shughuli zote zinafuata utaratibu, sheria na kanuni zilizowekwa ikiwemo kuangalia ubora na usafi unapatikani”Alisema

Alisema wanafanya hivyo ili kumuwezesha yule mchambuaji baada ya kumaliza taratibu zake aweze kupata kibali kama maborota yake yanapelekwa nje ya nchi apeleke kwa wakati kwa kukamailisha tararibu zote.

Mwisho.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...