Na Hamis Dambaya, DSM.

Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) imenunua tiketi 500 kwa ajili ya kulipia mashabiki 500 kuingia uwanja wa Benjamini Mkapa leo tarehe 22 agosti, 2025 kwa ajili ya kushuhudia mechi ya  robo fainali ambapo timu ya Tanzania -Taifa stars itacheza na Morocco majira ya saa mbili usiku katika uwanja wa Benjamini mkapa Dar es Salaam.

Akikabidhiwa tiketi hızo kwa niaba ya Kamishna wa Uhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro, Meneja wa idara ya huduma za utalii na Masoko Mariam Kobelo amesema kuwa uamuzi wa kuingiza mashabiki hao 500 una lengo la kuunga mkono juhudi za serikali za kuendeleza michezo na utalii pamoja na kuhamasisha watanzania kutembelea vivutio vya utalii vilivyopo nchini hususani hifadhi ya Ngorongoro.

Katibu Mkuu wa Baraza la Michezo Tanzania (BMT)  Neema Msita ameipongeza NCAA kwa uamuzi huo na kusema kuwa michuano ya fainali za Afrika kwa wachezaji wa ndani (CHAN) imevuta mashabiki wengi  katika nchi za Afrika na dunia kwa ujumla hivyo ni sehemu muhimu ya kutangaza vivutio vya utalii.

Taifa stars na Morocco zitachuana ijumaa hii katika hatua ya robo fainali ya michuano hiyo katika uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es salaam.





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...