Na Pamela Mollel,Arusha 

Meya wa Jiji la Arusha, Mheshimiwa Maximilian Matle Iranghe, ametoa tathmini ya ziara ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Mheshimiwa Riziki Shemdoe, iliyofanyika mkoani Arusha kwa lengo la kukagua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa ndani ya Jiji la Arusha.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Desemba 18, 2025, ofisini kwake, Meya Iranghe amesema ziara hiyo imelenga kupata picha halisi ya hatua za utekelezaji wa miradi pamoja na changamoto zinazojitokeza, hatua inayoiwezesha Serikali kutoa maelekezo ya haraka na sahihi kwa ajili ya kuboresha utekelezaji wake.

Ameeleza kuwa miongoni mwa miradi iliyokaguliwa ni ujenzi wa uwanja wa mpira pamoja na ujenzi wa soko jipya, miradi ambayo ni muhimu katika kukuza sekta ya michezo, biashara na kuchangia ukuaji wa uchumi wa wananchi wa Jiji la Arusha.

Kwa mujibu wa Meya Iranghe, Waziri wa TAMISEMI ameridhishwa na kasi ya utekelezaji wa miradi hiyo na kusisitiza kuwa hakuna sababu ya kuongeza muda wa utekelezaji wa miradi iliyopangwa. Waziri amewaelekeza wakandarasi na wasimamizi kuhakikisha wanazingatia viwango vya ubora na kukamilisha miradi kwa wakati uliopangwa.

Aidha, Meya Iranghe amebainisha kuwa ziara za viongozi wakuu wa Serikali zina mchango mkubwa katika kuongeza uwajibikaji kwa watendaji na kuimarisha usimamizi wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika mamlaka za serikali za mitaa.

Katika hitimisho lake, Meya Iranghe ameishukuru Serikali Kuu pamoja na wizara husika kwa kuendelea kutoa ushirikiano na ufuatiliaji wa karibu, akisisitiza kuwa Jiji la Arusha litaendelea kushirikiana na Serikali kuhakikisha miradi ya maendeleo inatekelezwa kwa ufanisi na kwa manufaa ya wananchi.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...