Na Mwandishi Wetu, Rombo.
Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) imeshiriki katika tamasha la _Rombo _Marathon_ lililofanyika leo tarehe 23 Desemba 2025, Rombo Mkoani Kilimanjaro na kuvutia wageni kutoka maeneo mbalimbali ya ndani na nje ya nchi.
Ushiriki wa Ngorongoro Rombo Marathon ambayo pia watumishi wa Mamlaka hiyo wameshiriki mbio za umbali tofauti inadhihirisha jitihada za mamlaka hiyo kuunga mkono sekta ya michezo, kutangaza vivutio vya utalii kupitia utalii wa michezo, kujenga uhusiano na wadau kupitia matukio ya kijamii na kitaifa na kimataifa.
Sambamba na kushiriki katika tamasha hilo, wananchi waliohudhuria mashindano hayo walipata fursa ya kutembelea banda la Ngorongoro lililowekwa mahsusi kwa ajili ya kutoa elimu kwa washiriki na wananchi kwa ujumla kuhusu shughuli za Uhifadhi na utalii pamoja na mchango wa hifadhi ya Ngorongoro katika kulinda urithi wa asili na wa kitamaduni.










Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...