JESHI la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia Furaha Mwile Nyelele, mkazi wa Kijiji cha Shilanga kwa tuhuma za mauaji ya mtoto wa jirani yake aliyekuwa Mwanafunzi wa Shule ya Msingi Shilanga darasa la saba aitwaye Boniventure Elia Lazaro [12] mkazi wa Shilanga.

Awali kabla ya tukio hilo tarehe 21.12.2025 saa 10:15 jioni huko Kijiji cha Shilanga, Kata ya Ilembo, Tarafa ya Isangati, Wilaya ya Mbeya Vijijini mtuhumiwa Furaha Mwile Nyelele alimpiga kwa kipande cha mti kichwani mtoto Boniventure Elia Lazaro [12] ambaye kwa sasa ni marehemu na kumsababishia jeraha ambapo alikimbizwa katika Hospitali Teule ya Ifisi kwa matibabu.

Tarehe 22.12.2025 saa 6:30 mchana akiwa anaendelea kupatiwa matibabu katika Hospitali Teule ya Ifisi alifariki dunia. Uchunguzi wa awali umebaini kuwa chanzo cha tukio hili ni kujichukulia sheria mkononi baada ya mtuhumiwa kumtuhumu mtoto kuiba mayai ya kuku.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linatoa kwa jamii kuacha tabia ya kujichukulia sheria mkononi ili kuepuka madhara. Aidha, wazazi na walezi wanakumbushwa kuzingatia suala la ulinzi na usalama wa mtoto kwa kuhakikisha haki za mtoto zinaheshimiwa na kulindwa.

Imetolewa na:
Kamanda wa Polisi,
Mkoa wa Mbeya.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...