Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umemtaka Mkandarasi Kampuni ya CCC International Engineering Nigeria Ltd anayetekeleza Mradi wa Kusambaza umeme katika Vitongoji 135 vya Majimbo 9 ya uchaguzi Mkoani Ruvuma kuongeza kasi ya ujenzi ili kukamilisha Mradi huo kwa wakati.
Meneja wa Usimamizi wa Miradi ya Kusambaza Umeme REA, Mha. Deogratius Nagu ametoa maelekezo hayo Januari 31, 2026 kwa nyakati tofauti wakati wa ziara ya kukagua utekelezaji wa Mradi katika Vitongoji vya Mlimani Park na Liuli Chini Wilaya ya Songea Mkoani wa Ruvuma.
"Kasi ya utekelezaji wa mradi huu hairidhishi kwani hadi sasa Mkandarasi yupo asilimia 56 wakati alipaswa kuwa ametekeleza kwa asilimia 80 kwa maana kwamba amewasha vitongoji 43 kati ya vitongoji 135 ambavyo alitakiwa kuwasha,” amefafanua Mha. Nagu.
Mhandisi Nagu amemuelekeza Mkandarasi kumbadilisha Meneja wa Mradi, kuhakikisha anaongeza timu za mafundi na wataalam katika maeneo yote ya mradi na aongeze usambazaji wa vifaa vya mradi ikiwemo transafoma na nyaya ili afanikishe kukamilisha mradi mapema zaidi.
“Tumeongeza nguvu ya ufuatiliaji hapa na tumemueleza haturidhishwi na kazi yake; ahakikishe anazingatia maelekezo yaliyotolewa leo, tumejipanga kumsimamia kwa karibu zaidi na tunaamini hadi mwezi wa sita atakuwa amekamilisha mradi,” amesema Mhandisi Nagu.
Kwa upande wake Mhandisi wa Mradi, Erick Njau akizungumza kwa niaba ya Meneja wa Mradi, Li Hongli amesema kuchelewa kwa mradi kunatokana na kuchelewa kufika kwa vifaa vya mradi hata hivyo aliahidi kutekeleza maelekezo na kukamilisha mradi kwa wakati.
"Ni kweli hatuna changamoto zaidi ya hii ya kucheleweshewa vifaa na watoa huduma, tumepokea maelekezo na tunaahidi kuongeza kasi,” amesema Mha. Njau.
Aidha, akizungumza kwa niaba ya Msimamizi wa Miradi ya REA Mkoa wa Ruvuma, Mhandisi Zakaria Ng’okorome amesema mradi unatekelezwa kwa gharama ya shilingi bilioni 14.56 na kwamba utanufaisha wateja wa awali zaidi ya 5,400.





Meneja wa Usimamizi wa Miradi ya Kusambaza Umeme REA, Mha. Deogratius Nagu ametoa maelekezo hayo Januari 31, 2026 kwa nyakati tofauti wakati wa ziara ya kukagua utekelezaji wa Mradi katika Vitongoji vya Mlimani Park na Liuli Chini Wilaya ya Songea Mkoani wa Ruvuma.
"Kasi ya utekelezaji wa mradi huu hairidhishi kwani hadi sasa Mkandarasi yupo asilimia 56 wakati alipaswa kuwa ametekeleza kwa asilimia 80 kwa maana kwamba amewasha vitongoji 43 kati ya vitongoji 135 ambavyo alitakiwa kuwasha,” amefafanua Mha. Nagu.
Mhandisi Nagu amemuelekeza Mkandarasi kumbadilisha Meneja wa Mradi, kuhakikisha anaongeza timu za mafundi na wataalam katika maeneo yote ya mradi na aongeze usambazaji wa vifaa vya mradi ikiwemo transafoma na nyaya ili afanikishe kukamilisha mradi mapema zaidi.
“Tumeongeza nguvu ya ufuatiliaji hapa na tumemueleza haturidhishwi na kazi yake; ahakikishe anazingatia maelekezo yaliyotolewa leo, tumejipanga kumsimamia kwa karibu zaidi na tunaamini hadi mwezi wa sita atakuwa amekamilisha mradi,” amesema Mhandisi Nagu.
Kwa upande wake Mhandisi wa Mradi, Erick Njau akizungumza kwa niaba ya Meneja wa Mradi, Li Hongli amesema kuchelewa kwa mradi kunatokana na kuchelewa kufika kwa vifaa vya mradi hata hivyo aliahidi kutekeleza maelekezo na kukamilisha mradi kwa wakati.
"Ni kweli hatuna changamoto zaidi ya hii ya kucheleweshewa vifaa na watoa huduma, tumepokea maelekezo na tunaahidi kuongeza kasi,” amesema Mha. Njau.
Aidha, akizungumza kwa niaba ya Msimamizi wa Miradi ya REA Mkoa wa Ruvuma, Mhandisi Zakaria Ng’okorome amesema mradi unatekelezwa kwa gharama ya shilingi bilioni 14.56 na kwamba utanufaisha wateja wa awali zaidi ya 5,400.







Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...