Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Clement Sangu, amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Kazi wa Qatar, Mhe. Dkt. Ali bin Saeed bin Samikh Al Marri, Jijini Riyadh, Saudi Arabia.
Katika mazungumzo ya viongozi hao, pande zote zimekubaliana kuimarisha ushirikiano katika masuala ya kazi na ajira, ikiwa ni pamoja na kubadilishana uzoefu, kukuza fursa za ajira na kulinda haki za wafanyakazi.
Vilevile, Ushirikiano huo umelenga kupanua fursa za ajira kwa Watanzania na kuendelea kuimarisha mahusiano ya kidiplomasia kati ya Tanzania na Qatar.


Katika mazungumzo ya viongozi hao, pande zote zimekubaliana kuimarisha ushirikiano katika masuala ya kazi na ajira, ikiwa ni pamoja na kubadilishana uzoefu, kukuza fursa za ajira na kulinda haki za wafanyakazi.
Vilevile, Ushirikiano huo umelenga kupanua fursa za ajira kwa Watanzania na kuendelea kuimarisha mahusiano ya kidiplomasia kati ya Tanzania na Qatar.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Clement Sangu, akizungumza na Waziri wa Kazi wa Qatar, Mhe. Dkt. Ali bin Saeed bin Samikh Al Marri, walipokutana katika kikao cha pembeni (side meeting) wakati wa mkutano wa Mawaziri wa Kazi (Global Labour Market Cinference) unaofanyika Jijini Riyadh, Saudi Arabia.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...