Katibu Mkuu wa Women Political Leaders (WPL), Neema Lugangira, amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi Claver Gatete, Katibu Mtendaji wa Tume ya Umoja wa Mataifa ya Uchumi kwa Afrika (United Nations Economic Commission for Africa).

Wawili hao wamejadiliana kuhusu mchango wa lishe katika maendeleo ya kiuchumi na umuhimu wa Serikali za Afrika kuipa lishe uzito wa kimkakati sawa na sekta nyingine za ukuaji.

Pia, wameangazia jinsi teknolojia za kidijitali na teknolojia mpya kama akili mnemba AI zinavyoweza kuharakisha maendeleo; na nafasi ya viongozi wanawake katika kuongoza ajenda hii hivyo kuchangia ukuaji wa kiuchumi barani Afrika.

Wamekutana leo jijini Addis Ababa, nchini Ethiopia.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...