Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (ADEM), Dkt. Maulid J. Maulid, akimkabidhi cheti cha ushiriki wa Mafunzo ya Usimamizi wa Kimkakati wa Elimu Mwalimu Dennis John Otieno, ambaye ni Mwenyekiti wa Umoja wa Wakuu wa Shule za Sekondari Tanzania (TAHOSSA) na pia Mkuu wa Shule ya Sekondari Ilboru mkoani Arusha.

Mafunzo hayo ya Uongozi kwa Viongozi wa Elimu na Wakuu wa Shule yamefanyika katika chuo cha Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (ADEM) kilichopo Bagamoyo.

Akizungumza wakati wa kufunga mafunzo hayo, Dkt. Maulid aliwapongeza washiriki kwa kujituma na kuonesha uzingatiaji mkubwa katika vipindi vya mafunzo. Aliwataka kuyazingatia na kuyatekeleza kwa vitendo maudhui waliyojifunza ili kuleta tija katika usimamizi wa taaluma, malezi na utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika taasisi zao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...