Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiondoka nchini kuelekea Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) leo tarehe 02 Februari, 2026, ambapo atashiriki kwenye mkutano wa World Government Summit (WGS 2026) na uzinduzi wa Global Africa Investment Summit (GAIS).
Ushiriki wa Tanzania katika WGS 2026 unaakisi utekelezaji wa DIRA 2050 na Sera Mpya ya Mambo ya Nje, zinazoweka diplomasia ya kiuchumi kama nguzo ya mahusiano ya kimataifa.
Lengo ni kuoanisha sera, ushirikiano na mitaji ya uwekezaji kwa maendeleo ya taifa.






Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...