NA EMMANUEL MBATILO, MICHUZI TV

KLABU ya Simba imelazimishwa sare 2-2 na Esperance de Tunis katika mchezo wa hatua ya makundi ligi ya mabingwa Afrika.

Katika mchezo huo Simba Sc ilifanikiwa kuongoza kwa mabao 2-0 kipindi cha kwanza kupitia kwa Shomari Kapombe na Yusuf Kagoma na kwenda mapumziko wa wakiwa mbele.

Kipindi cha pili Esperance de Tunis waliingia wakilisaka lango la Simba sc nakufanikiwa kupata bao la kwanza baada ya Lassane Kante kutoa basi ambayo ilimpata mpinzani na kwenda kufunga bao ambalo liliwapa matumaini na kufanikiwa kupata bao la pili.

Kwenye mchezo huo pia Esperance de Tunis walipata penati dakika ya za mwisho wa mchezo lakini penati hiyo hawakuweza kupata bao.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...