Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inashiriki Mkutano wa 48 wa Baraza la Mawaziri Afrika unaofanyika jijini Addis Ababa, Ethiopia kuanzia Februari 11-12, 2026. Ujumbe wa Tanzania katika mkutano huo unaongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe.shimiwa Mahmoud Thabit Kombo (Mb).

Mkutano huo unawakutanisha Mawaziri wa Mambo ya Nje na viongozi waandamizi kutoka nchi wanachama wa Umoja wa Afrika kujadili masuala muhimu ya maendeleo, usalama, ushirikiano wa kikanda na utekelezaji wa maamuzi ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali.

Akifungua mkutano huo, Mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika (AUC), Mhe. Mahmoud Youssouf Ali, amesisitiza umuhimu wa mageuzi ya Taasisi na umuhimu wa amani na maendeleo barani Afrika kuelekea Mkutano wa 39 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa AU.

Amesema kuwa, Mageuzi yanaendelea chini ya Mpango wa 2024–2028 na kubainisha mafanikio yaliyopatikana katika kuimarisha muundo wa amani na usalama, kuhakikisha ufadhili endelevu, pamoja na kuimarisha taasisi za Umoja huo. Ameishukuru Jamhuri ya Angola kwa uongozi wake wa Baraza la Utendaji, huku Angola ikiwa ni Mwenyekiti wa Umoja huo anayemaliza muda wake.

Akizungumza katika ufunguzi wa mkutano huo, Waziri wa Mambo ya Nje wa Ethiopia Mhe. Gedion Timothewos, ameeleza kuwa mabadiliko yanayoendelea katika siasa za kimataifa yanazidi kudhoofisha misingi ya ushirikiano wa kimataifa na mfumo wa ushirikiano wa kimataifa.

Naye Katibu Mtendaji wa Tume ya Umoja wa Mataifa ya Uchumi ya Afrika (UNECA) Mhe.Clever Gatete ameongelea utafutaji fedha kwa ajili ya miradi ya maendeleo kwa nchi wanachama, kuunganisha miundombinu ya uzalishaji, kuongeza thamani ya madini na mazao, kuimarisha soko huru barabi Afrika na kutumia maarifa na teknolojia ya sasa ili kupata maendeleo.

Mkutano huo wa ngazi ya juu wa mawaziri ni sehemu ya maandalizi kwa ajili ya Kikao cha 39 cha Kawaida cha Wakuu wa Nchi na Serikali




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...