
LEO hii Meridianbet tunaangazia klabu ya Simba ambayo imekuwa na mabadiliko yanayotokea hap na pale huku nafasi ya wao kushinda taji la NBC Premier League inakuwa ngumu zaidi.
Kwenye ligi kuu ya Tanzania yaani (NBC Premier League), Simba imekuwa ikikumbwa na mwenendo usio thabiti wa matokeo. Kumekuwa na vipindi vya ushindi vinavyofuatwa na matokeo yasiyoridhisha, hali iliyosababisha kupoteza alama muhimu kwenye mbio za ubingwa.
Hata hivyo, pamoja na changamoto hizo, timu imeendelea kuonyesha ari ya kupambana na haijakata tamaa katika malengo yake ya kumaliza msimu katika nafasi ya ushindani.
Nikisema huu ni msimu mbaya kwa Simba namaanisha pia kule kwenye michuano ya CAF timu hii imeshindwa kuendelea mbele baada ya kutolewa kwenye hatua ya Makundi wakikusanya pointi 5 pekee wakishika nafasi ya mwisho kwenye Kundi.
NB: Mbali na kubashiri mechi za kandanda, Meridianbet pia inakupa nafasi ya kucheza michezo ya kasino mtandaoni kama Aviator, Keno, Super Heli, ambapo unaweza kujishindia zawadi kama simu mpya aina ya Samsung A26. PIGA *149*10# AU tembelea tovuti yao meridianbet.co.tz
Kuaga mapema mashindano ya kimataifa kumekuwa pigo, lakini pia kumezua tafakuri ya kina ndani ya klabu kuhusu mwelekeo na maboresho yanayohitajika.
Benchi la ufundi limekuwa likifanya tathmini ya kina kuhusu kikosi, likitafuta uwiano bora kati ya wachezaji wazoefu na wale chipukizi. Pia, klabu imekuwa ikifanya jitihada za kurekebisha mapungufu yaliyojitokeza katika safu ya ulinzi na umaliziaji wa nafasi za mabao. Mabadiliko ya kimfumo na kiufundi yanatarajiwa kuleta uthabiti zaidi katika mechi zijazo.
Pamoja na kuondolewa CAF, Simba chini ya kocha mkuu Steve Barker sasa ina nafasi ya kuelekeza nguvu zake zote katika mashindano ya ndani, ikiwemo ligi na Kombe la Shirikisho. Hii ni fursa ya kurejesha imani ya mashabiki kupitia matokeo chanya na kuonyesha kuwa klabu ina uwezo wa kusimama tena katika nyakati ngumu.
Kwa ujumla, msimu huu ni kipindi cha kujifunza na kujipanga upya kwa Simba SC. Historia ya klabu inaonyesha kuwa imewahi kupitia changamoto na kurejea kwa nguvu zaidi.
Pia klabu hiyo imefanya usajili wa wachezaji wapya ndani ya kikosi dirisha dogo la usajili akiwemo Loemba, Gueye, Ouara, Toure, Kibabage na wengine wengi ambao wamkuja kuleta mabadiliko ndani ya klabu.
Baada ya kutoa suluhu kwenye Karikaoo Derby sasa Simba wana pointi 24 wakiachwa pointi 5 na vinara wa ligi Yanga ambao wana pointi zao 29. Je Mnyama msimu huuu atachukua Kombe gani? ODDS KUBWA zipo Meridianbet.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...