Mhe Mbunge wa Jimbo la Mlimba,Dkt KellenRose Rwakatare, ametembelea mabinti 300 wanaosoma katika Chuo cha Maendeleo FDC Ifakara na kuwapatia mahitaji mbalimbali muhimu kwa ajili ya kuendeleza masomo yao ya ufundi stadi.

Ziara hiyo imelenga kuwatia moyo, kuwasikiliza pamoja na kuthibitisha dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan katika kuwawezesha vijana wa kike kielimu na kiuchumi.

Akizungumza na mabinti hao, Mhe Mbunge aliwahimiza kusoma kwa bidii, kutumia vyema fursa waliyoipata na kuwa chachu ya mabadiliko katika jamii. Ziara hiyo pia ilisindikizwa na viongozi mbalimbali wa Wilaya ya Kilombero waliopongeza juhudi hizo za maendeleo




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...