SERIKALI imethibitisha kuwa ipo katika mazungumzo na mwekezaji mwingine kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa barabara ya haraka (expressway) kutoka Dar es Salaam hadi Chalinze.

Akizungumza katika mjadala maalum kuhusu namna Kituo cha Ubia kati ya Sekta ya Umma na Binafsi (PPPC) kinavyofanya kazi, Mkurugenzi wa kituo hicho, David Kafulila, alisema hatua hiyo inalenga kuhakikisha mradi unatekelezwa kwa ufanisi na kwa gharama nafuu.

Alieleza kuwa Serikali ililazimika kuachana na mkandarasi wa awali baada ya kubainika kuwa gharama alizowasilisha zilikuwa mara mbili zaidi ya makadirio yaliyokubalika.

Kafulila aliongeza kuwa mchakato wa kumpata mwekezaji mpya unaendelea, huku Serikali ikiweka mkazo katika kupata mbia atakayetoa huduma bora kwa kuzingatia thamani halisi ya fedha.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...