Na Mwandishi Wetu
Wanawake wa Tume ya Ushindani (FCC ) wametakiwa kuwa na upendo ambao utajenga mshikamano na kuleta ufanisi katika Taasisi.
Hayo ameyasema Mwakilishi wa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC, Bi. Magdarena Utouh katika Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ambayo hufanyika kila Machi 8 ya kila mwaka.
Magdelena amesema maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ni ishara ya kufanya wanawake kuwa na nguvu ambayo inatoa mchango katika Taifa pamoja na kuchochea maendeleo.
Amesema kuwa maadhimisho hayo ni pamoja ya kupeleka ujumbe kwa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kuwa tuko nyuma yake na tunapiga kazi.
Aidha amesema.kuwa wanawake ni jeshi kubwa hivyo tunahitaji kuendelea kujituma na kuleta matokeo katika maeneo yetu ya kazi.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...