Na Mwandishi Wetu

Wanawake wa Tume ya Ushindani (FCC ) wametakiwa kuwa na  upendo ambao utajenga mshikamano na kuleta ufanisi katika Taasisi.

Hayo ameyasema Mwakilishi wa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC, Bi. Magdarena Utouh katika  Maadhimisho  ya Siku ya  Wanawake Duniani ambayo hufanyika kila Machi 8 ya kila mwaka.

Magdelena amesema maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ni ishara ya kufanya wanawake  kuwa na  nguvu ambayo inatoa mchango katika Taifa pamoja na kuchochea maendeleo.

Amesema kuwa maadhimisho hayo ni pamoja ya kupeleka ujumbe kwa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kuwa tuko nyuma yake na tunapiga kazi.

Aidha amesema.kuwa wanawake ni jeshi kubwa hivyo tunahitaji  kuendelea kujituma na kuleta matokeo  katika maeneo yetu ya kazi.

Kauli mbiu ya mwaka ya  Maadhimisho  ya Siku ya Wanawake Duniani  2026 ni Haki na Usawa kwa Wanawake na Wasichana: Msingi Jumuishi kufikia Dira 2050.











 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...