WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba, leo Machi 13, 2026 ameweka jiwe la msingi la Mradi wa Maji wa Miji 28 katika Kata ya Shanwe, Manispaa ya Mpanda mkoani Katavi.
Mradi huo wenye thamani ya shilingi bilioni 22.8 umefikia asilimia 55 ya utekelezaji na unatarajiwa kukamilika Julai 2026. Kukamilika kwake kutasaidia kuongeza upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama kwa wananchi wa eneo hilo.
Baada ya kukagua maendeleo ya mradi huo, Dkt. Mwigulu amemtaka mkandarasi kuhakikisha anaukamilisha kwa wakati na kwa ubora uliokusudiwa ili wananchi waanze kunufaika na huduma ya maji.
Mradi huo unatarajiwa kuzalisha takribani lita milioni 12 za maji kwa siku.










Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...