Wito umetolewa kwa wawekezaji na wazalishaji nchini kutumia huduma za Shirika la Viwango Tanzania (TBS), hususan katika sekta ya vipimo (metrolojia), kutokana na kutambulika kwake kimataifa.

Akizungumza na wanahabari Aprili, 2, 2026 jijini Dar-es-Salaam, Afisa Mkuu wa Metrolojia Joseph Kadenge kutoka Shirika la Viwango Tanzania (TBS) amesema kuwa Metrolojia (Sayansi ya Vipimo) ni Moja ya Misingi minne ya Ubora inayoangalia ubora wa vipimo katika mashine zinazotumika katika uzalishaji.

Amesema ubora wa bidhaa unaanzia kwenye mashine zinazozalishia, kama mashine hazina vipimo sahihi basi hata ubora wa bidhaa uko mashakani.

Kadenge ameongeza kuwa TBS ina Maabara ya Taifa (National Metrology Laboratory) ya Vipimo inayotambulika kimataifa kupitia Shirika la Vipimo Duniani (BIPM), huku uwezo wake wa upimaji ukiwa umeorodheshwa katika kanzidata ya kimataifa.

Aidha, maabara hizo zimepata ithibati ya umahiri kutoka taasisi ya kuangalia umahili ya nchi za SADC inayoitwa SADCAS, hatua inayothibitisha ubora wa huduma zake na kuwahakikishia wawekezaji kuwa huduma za vipimo zinapatikana kwa viwango vinavyokubalika kimataifa.

Kupitia umahiri huo, Kadenge ametoa wito kwa wawekezaji na wazalishaji kutokuwa na hofu ya kuwekeza Tanzania kwani upatikanaji wa huduma ya Ugezi (Calibration) zinapatikana kwa urahisi.





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...