Jeshi la Polisi Tanzania lingependa kujulisha kuwa, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Camillus Wambura, amemhamisha Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Twaha Juma Lulengelule ambaye alikuwa Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (RCO) Mkoa wa Tabora kuwa Kamanda wa Polisi (RPC) Mkoa wa Tabora.


Uhamisho huo umefanyika ili kujaza nafasi iliyokuwa wazi baada ya aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa huo, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Richard George Abwao, kufariki dunia Juni 20, 2026.


Imetolewa na;

Msemaji wa Jeshi la Polisi

Makao Makuu ya Polisi

Dodoma,Tanzania
Next
This is the most recent post.
Previous
Older Post

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...