Na Said Mwishehe,Michuzi TV

JUBILEE Group Tanzania imezindua rasmi ukuta uliojengwa kuzunguka Shule ya Msingi Madenge iliyopo Temeke, Dar es Salaam lengo likiwa kutatua ya usalama na changamoto ya usumbufu uliokuwa ukiababishwa na usumbufu wapita njia hali iliyokuwa ikiathiri mazingira bora ya kufundishia na kujifunzia.

Hivyo kujengwa kwa ukuta huo wanaamini utachangia kuimarisha mazingira salama na tulivu ya elimu, hivyo kuwapa walimu nafasi bora ya kufundisha na wanafunzi mazingira mazuri ya kujifunza na kufanya vizuri kitaaluma.

Uzinduzi huo uliozinduliwa leo Agosti 7,2026 katika shule hiyo umehudhuriwa na maofisa Watendaji Wakuu wa Jubilee Life Insurance na Jubilee Health Insurance, Bi. Helena Mzena na Dkt. Harold Adamson, pamoja na viongozi wa serikali za mitaa, uongozi wa shule na wafanyakazi wa Jubilee Group Tanzania.

Jubilee Group Tanzania itaendelea kutekeleza shughuli za uwajibikaji kwa jamii (CSR) kwa lengo la kuleta mchango chanya katika elimu, afya na ustawi wa jamii, kwa kuamini kwamba jamii yenye maendeleo ndiyo msingi wa maendeleo endelevu ya taifa.

Awali akisoma risala ya shule ya msingi Madenge wilayani Temeke Mwalimu Edith Mchome amesema wanashukuru kujengewa ukuta huo na hivyo kuondokana na changamoto mbalimbali ambazo wanafunzi na walimu walikuwa wakizipata kwa kutokuwa na uzio.

“Kwa niaba ya wanafunzi wote wa shule ya msingi Madenge, tunayofuraha kubwa kutoa shukrani zeiu za dhati kwa "jubilee Insurance Life kuiwezesha shule yetu kujengewa uzio upande mmoja korofi sana, ambape hapo awali hatukuweza kusoma kwa uskivu nautuivu.

“Jubilee Insurance Life imeturejeshea utulivu na usikivu katika mazingira yetu ya shule

kwa upande huo wenye uzio huu.Kabla ya ukuta huu ambao sasa tuko salama na hakuna tena vurugu za wapita njia wala wavuta bangi waliokuwa wanakuja hapa shuleni.

“Pia tunashukuru kwa kutupatia msitu ambao umetusaidia kutunza mazingira yetu ya shule ambayo yamekuwa kivutio kama mlivyoona, msitu huo umetusaidia sisi wanafunzi na

walimu wetu kujikinga dhidi ya upepo mkali na hivyo kuepusha athari zaidi za upepo mkali.

“Pamoja na hayo msitu umetusaidia kupata hewa safi ambayo tumekuwa tukiifurahia kila siku,”amesema Mchome na kuongeza pia wanawashukuru Jubilee Insurance Life kwa kutuwezesha kupata vifaa vya usafi kama vile reki, majembe na fyekeo. Vifaa hivyo vinaendelea kuwasaidia kutunza mazingira yao na kuyafanya kuwa safi kila siku kama mnavyoshuhudia.”




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...